LIONEL MESSI AIONGOZA BARCELONA KUISULUBISHA 3-0 JUVENTUS

ndondo2017.blogspot.com
Michuano ya Ligi ya Mabingwa imeanza kwa ushindi kwa Manchester United, Barcelona, PSG na Chelsea, Messi akiendelea kutoa burudani ya soka
Lionel Messi alitikisa nyavu mara mbili Barcelona ikitoka kifua mbele kwa ushindi wa 3-0 dhidi ya Juventus mechi ya kwanza Ligi ya Mabingwa msimu wa 2017-18, kadhalika Paris Saint-Germain, Manchester United na Chelsea zilipata ushindi mnono Jumanne.
Baada ya msimu wa majira ya joto uliojaa adha tele, Barca walikabiliana na mshindi wa pili wa michuano hiyo msimu uliopita, huenda hawakucheza katika kiwango walichotaka kama timu, lakini Lionel Messi alidhihirisha umahiri wake akiiwezesha Blaugrana kushinda pointi tatu muhimu.
Mchezaji mpya Ousmane Dembele alipewa nafasi kikosi cha kwanza Camp Nou, lakini ni Messi aliyeweka kimiani bao la kufungua ukurasa baada ya kugongeana vema kabisa na Luis Suarez.

No comments:

Post a Comment

Alichofanyiwa Rudiger na shabiki wa Chelsea

Kufatia mchezo wa jana kati ya Man city na Chelsea, Chelsea kuambilia kipigo cha goli 6, baada ya mchezo kumalizika mlinzi huyo wa kat...

Most viewed