GOLI LA MAROUANE FELLAINI DHIDI YA BASEL LATHIBITISHA UMUHIMU WAKE

ndondo2017.blogspot.com
Marouane Fellaini ameonyesha ni kwa nini bado ni mchezaji muhimu kwenye kikosi cha Manchester United baada ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Basel
"Namhitaji." Hayo yalikuwa maneno ya Jose Mourinho kuhusu Marouane Fellaini kabla ya mechi ya Manchester United Ligi ya Mabingwa dhidi ya Basel Jumanne.
Haikumchukua muda mrefu kiungo huyo kuonesha ni kwa nini anahitajika, akiingia kutokea benchi baada ya Paul Pogba kupata majeraha dakika ya 18 ya mchezo aliipatia bao la kwanza United iliyoshinda 3-0 Old Trafford.
Fellaini alionesha vitu vingi zaidi ya goli alilofunga. Alimsaidia Nemanja Matic alipopoteza mpira katika mazingira ya hatari, lakini pia alipiga krosi maridadi kwa Marcus Rashford aliyefunga ukurasa wa mabao dhidi ya Basel.

No comments:

Post a Comment

Alichofanyiwa Rudiger na shabiki wa Chelsea

Kufatia mchezo wa jana kati ya Man city na Chelsea, Chelsea kuambilia kipigo cha goli 6, baada ya mchezo kumalizika mlinzi huyo wa kat...

Most viewed