Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema kuwa timu yake haijafanya chochote katika mbio za taji Ligi Kuu Uingereza.
United wameshinda mara sita na sare moja katika mechi zao saba za msimu huu, ingawa bado hawajakabiliana na wapinzania wanaoaminika kuwa washindani halisi wa taji.
Mourinho amekiri kuwa timu yake imeanza vizuri, lakini amesisitiza kuwa bado kuna kazi kubwa mbeleni ikiwa klabu hiyo inataka kuendelea kubaki kileleni.

No comments:
Post a Comment