OSCAR AMESEMA BADO ANA MATUMAINI YA KUREJEA CHELSEA KWA SIKU ZA BAADAYE

Kiungo wa Brazil, Oscar amesema kuwa anataka kurudi Ligi ya Uingereza kabla ya kufikisha umri wa miaka 30 na ana matumaini ya kujiunga tena na Chelsea
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 aliondoka Stamford Bridge kwa dau kubwa la fedha kwenda Ligi Kuu la China mwezi Januari, aliigharimu klabu ya Shanghai SIPG paundi millioni 60 kuinasa saini yake.
Oscar amekuwa na fomu nzuri kwa sasa, akiwa sehemu ya kikosi cha kwanza amefaniki kufunga mabao tisa katika mechi 17 kwa Red Eagles, lakini tayari ameshaanza kuifikiria kurejea klabu yake ya zamani Chelsea zaidi chini ya mstari.

"Ndiyo, nitarejea. Mimi bado ni mdogo, nina umri wa miaka 26," aliiambia Premier League Brasil. "Ni nani anayejua, katika miaka miwili au mitatu kurudi Ligi Kuu ya Uingereza ... Nitakuwa na furaha sana.Na hasa kwa Chelsea, ambayo imenifungulia milango ya kurudi."

No comments:

Post a Comment

Alichofanyiwa Rudiger na shabiki wa Chelsea

Kufatia mchezo wa jana kati ya Man city na Chelsea, Chelsea kuambilia kipigo cha goli 6, baada ya mchezo kumalizika mlinzi huyo wa kat...

Most viewed