MVUNJA REKODI RASHFORD ANAWEZA KUWA GWIJI WA MANCHESTER UNITED

Mshambuliaji huyo wa Uingereza ameendeleza mwendo wake mzuri mbele ya goli katika ushindi wa 4-0 Carabao Cup dhidi ya Burton Albion
Manchester United walipata ushindi kwenye Kombe la Carabao Jumatano, Marcus Rashford akifunga mabao mawili ya mapema na kutoa pasi moja ya goli wakiitungua 4-0 Burton Albion katika uwanja wa Old Trafford.
Kinda huyo sasa ameifungia United mabao 24 na bado hajatimiza miaka 20, kiwango chake cha msimu huu ni ishara kuwa amepevuka.
Hata Wayne Rooney hakuweza kufunga mabao mengi kwa klabu akiwa na umri wa Rashford, na nahodha huyo wa zamani wa Uingereza aliweka rekodi ya magoli 253 kabla ya kurejea Everton majira ya joto.
Awali, alitabiriwa na Jose Mourinho kuwa ataikaribia rekodi ya Rooney, Rashford ameendelea kuwa mshambuliaji mahiri.
Na mwandishi  wa Manchester United Kris Voakes anasema, ikiwa bado n siku za mapema sana kwa Rashford, ameonesha dalili zote za kuwa shujaa wa United sambamba na magwiji wa miaka iliyopita.

RONALDO ANATAKA MSHAHARA SAWA NA MESSI

Ronaldo anavuna paundi millioni 19. 5m kwa mwaka, na kumfanya awe mchezaji anayelipwa kuliko wote klabuni.
Mchezaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ameripotiwa kudai ongezeko la mshahara.
Straika huyo wa Ureno anataka kuongeza mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya paundi  millioni 27m kwa mwaka na kuwa sawa dhidi ya mpinzani wake wa  Barcelona Lionel Messi, chanzo ni kutoka Sun.
Ronaldo yupo chini ya mkataba na mabingwa hao wa La Liga hadi 2021 na tayari anavuna paundi millioni 19. 5m kwa mwaka, na kumfanya awe mchezaji anayelipwa kuliko wote klabuni.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 alirudi kutoka kufungoni siku ya Jumatano jioni ili kukabiliana na Real Betis kwenye Bernabeu, mechi ambayo klabu yake ilifungwa goli moja kwa bila.
Ripoti zilizopita zinaonyesha kuwa Daudi Beckham anaweza kujaribu kumshawishi Ronaldo kujiunga na timu yake ya Miami katika Ligi Kuu ya Soka wakati mkataba wake wa Real ukifika kikomo.

LIVERPOOL ITAWEZA KUPINDUA MBELE YA LEICESTER CITY KING POWER?


Leicester wameifunga Liverpool katika mechi tatu za mwisho walizokutana King Power - mechi ya mwisho kabisa ikiwa Kombe la EFL Jumanne usiku
Liverpool wanataka kukomesha mwendo wa mechi nne bila ushidi katika michuano yote watakaposafiri kwenda Leicester City kwenye Ligi Kuu Uingereza Jumamosi mchana.
Mechi hiyo inakuja tena ikiwa ni siku nne tu tangu timu hizo zikutane kwenye mechi ya Kombe la EFL, Leicester wakiibuka na ushindi wa 2-0 katika ardhi ya nyumbani kwao na kutinga raundi ya 16.
Haipingiki kwamba Leicester walikuwa kwenye wakati mgumu kupata matokeo katika hatua za mwanzo kampeni za 2017-18, lakini Foxes wamekumbana na mechi ngumu sana.
Walichezea kichapo cha 4-3 dhdi ya Arsenal katika mechi ya ufunguzi wa msimu, lakini walirejea kwenye njia za ushindi baada ya kushinda 2-0 dhidi ya Brighton & Hove Albion.
Foxes walipoteza mchezo dhidi ya Manchester United na dhidi ya Chelsea kwenye uwanja wa nyumbani, kabla ya kupata sare ya 1-1 Huddersfield Town wikiendi iliyopita. Jumla ya pointi nne tu kutoka kwenye mechi tano, na wanashika nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi.
Lakini jambo la kuogopesha ni kwamba Leicester wamecheza mechi moja tu bila kuruhusu goli na wameruhusu magoli 18 katika mechi nane za mwisho Ligi Kuu Uingereza, na ikiwa watapoteza mechi wikiendi hii watafikia idadi ya pointi ndogo zaidi walizowahi kupata katika mechi sita Uingereza.

Vijana wa Shakespeare wataingia dimbani wakiwa na ari wakitaka kuonyesha kuwa ushindi wa 2-0 waliopata dhidi ya Liverpool kwenye Kombe la EFL haukuwa wa kubahatisha.
Liverpool wamejikusanyia pointi saba kutoka kwenye mechi tatu za mwanzo katika msimu wa Ligi Kuu Uingereza wa 2017-18, na mambo yalikuwa murua pale waliposhinda mabao 4-0 dhidi ya Arsenal Agosti 27.
Tangia hapo, kikosi cha Jurgen Klopp kimeshindwa kupata ushindi katika mechi nne kwenye michuano mitatu tofauti. Reds walinyukwa 5-0 Manchester City baada ya mapumziko, kabla ya kupata sare dhidi ya Sevilla na Burnley kwenye Ligi ya Mabingwa na Ligi ya Uingereza mtawalia.
Liverpool imeshinda pointi 132 katika mechi 73 chini ya Klopp, ambazo ni pointi tisa pungufu katika kipindi sawa chini ya Brendan Rodgers ambaye alitupiwa virago kama kocha mkuu Oktoba 2015.

GUARDIOLA: CITY HAINA UHAKIKA WA KUIFUNGA PALACE

Safari ya Palace kwenda City ni mwanzo wa ratiba ngumu ambayo mbele yake watakutana na Manchester United na Chelsea
Meneja wa Manchester City Pep Guardiola amesema kuwa anaiheshimu sana Crystal Palace inayohaha katika kampeni za Ligi Kuu Uingereza kuelekea mechi yao katika uwanja wa Etihad Jumamosi.
Eagles wamekuwa na mwanzo mbaya msimu huu katika historia yao kwenye Ligi Kuu, wakiwa wamepoteza mechi tano za mwanzo bila kufunga hata goli moja.
Kocha wa zamani wa Uingereza Roy Hodgson alichukua mikoba ya Frank de Boer kama meneja wa Palace wiki iliyopita lakini alishindwa kuleta mabadiliko ya haraka timu hiyo ikiambulia tena kipigo cha 1-0 dhidi ya Southampton katika Selhurst Park.
City wapo kileleni mwa msimamo wa ligi na wameshinda mechi zao tatu za mwisho katika michuano yote kwa jumla ya magoli 15-0, lakini Guardiola amesisitiza kuwa ushindi dhidi ya timu ya Hodgson si jambo la uhakika.
"Naheshimu sana kile nilichokiona kutokakwa Palace dhidi ya Southampton na Burnley," aliwaambia wanahabari Ijumaa mchana. "Wametengeneza nafasi nyingi. Niliwaonyesha wachezaji wangu nafasi zote walizotengeneza, katika mechi mbili tu. Wataingiza mipira mingi mirefu ndani ya boksi na krosi.
"Namkubali Roy Hodgson, amekuwa akishughulika na soka muda mrefu na anastahili kupewa heshima yake. Napenda nguvu alizo nazo na ni mzoefu na soka la Ulaya."
Safari ya Palace kwenda City ni mwanzo wa ratiba ngumu ambayo mbele yake watakutana na Manchester United na Chelsea.

POGBA ANAWEZA KUWA NJE WIKI 12 AU SIKU 12 - MOURINHO

Jose Mourinho amethibitisha kuwa Manchester United bado hawana uhakika ni muda gani itamchukua Paul Pogba kupona majeraha.

MCHEZAJI BORA WA WIKI NI EMMANUEL OKWI


Okwi amefikisha magoli 6 katika michezo miwili aliyoicheza mpaka sasa ya Ligi Kuu
Mshambuliaji wa Simba, raia wa Uganda, Emmanuel Okwi amefanikiwa kuibuka mchezaji bora wa wiki baada ya kuwaiwezesha klabu yake kuibuka na alama tatu muhimu, kwenye ushindi wa goli 3 kwa bila dhidi ya Mwadui.
Okwi amefanikiwa kuibuka nyota bora wa wiki baada ya kuwafunika wachezaji wengine waliokuwa na wikendi nzuri kama Peter Mapunda wa Majimaji, Katsvairo wa Singida United na wengine waliokuwa na kiwango bora.
Katika mchezo huo na Mwadui, Mganda huyo alikuwa mwiba mkali kwa safu ya ulinzi wa Mwadui,  alifanikiwa kufunga mabao mawili dakika ya ( 7, 60 ) kwa mashuti ya umbali wa mita 25 ambayo yalimshinda mlinda mlango wa wa Mwadui, Arnold Massawe.

ALAN SHEARER: "LIVERPOOL HAINA TOFAUTI YOYOTE CHINI YA JURGEN KLOPP"

Safu ya beki ya Liverpool imekuwa dhaifu kiasi cha kuwakera mashabiki wengi wa klabu hiyo na Alan Shearer amedai kuwa Klopp ameshindwa kutatua tatizo
Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Uingereza Alan Shearer amedai kuwa Liverpool "haina tofauti" baada ya kuwa chini ya meneja wa sasa Jurgen Klopp ukilinganisha na ile iliyokuwa chini ya bosi wa Celtic Brendan Rodgers.
Rodgers alitupiwa virago na Liverpool Oktoba 2015 kufuatia madai kuwa kocha huyo raia wa Ireland hakuweza kutatua matatizo ya beki mbovu iliyokuwa ikiruhusu magoli kizemmbe, na kuigharimu timu kupoteza pointi zaidi.
Klopp aliiongoza Liverpool hadi kumaliza nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Ku Uingereza msimu uliopita, lakini kiulizo bado kipo kuhusu safu ya ulinzi ya Liverpool, ambayo tayari imesharuhusu magoli tisa katika ligi msimu huu.
"Naam, amewarejesha kwenye Ligi ya Mabingwa baada ya kutinga nafasi ya nne msimu uliopita, jambo ambalo limempa sifa nyingi," Shearer aliandika katika kolamu yake kwenye The Sun.
"Ukweli, ni kwamba, Liverpool haina tofauti yoyote chini ya Klopp zaidi ya ilivyokuwa chini ya Brendan Rodgers, kweli wanakimbia sana mbele, lakini nyuma hawana ujanja."
Liverpool hawajashinda mechi tatu za mwisho katika michuano yote, na walishikiliwa kwa sare ya 1-1 na Burnley kwenye Ligi Kuu Uingereza Jumamosi mchana.

WACHEZAJI WA REAL MADRID HAWAMTAKI ALEXIS SANCHEZ

Kwa mujibu wa habari kutoka Hispania, wachezaji wa Real Madrid wameutaka uongozi wa klabu hiyo kuachana na mpango wa kumsajili Alexis Sanchez
Imeripotiwa kuwa viongozi wa Real Madrid wamezuiliwa kufanya mchakato wa kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, kwani wachezaji wa Los Blancos wameweka bayana kuwa hawamtaki mchezaji huyo wa kimataifa wa Chile Bernabeu.
Inaaminika kuwa nyota huyo wa Arsenal alikuwa kwenye rada za Los Blancos kuelekea msimu ujao wa majira ya joto, ambapo atakuwa akipatikana kama mchezaji huru.
Kwa mujibu wa chanzo cha Hispania Don Balon, hata hivyo, mchezaji huyo amekanusha kuwa hana ndoto hiyo ya kuhamia Bernabeu kwa sababu amewahi kucheza Barcelona.
Sanchez ambaye amedumu miaka mitatu Camp Nou kabla ya kujiunga na Arsenal 2014, inaaminika alikuwa akikomaa kutua aidha Madrid au Manchester City.
Imedai kuwa nahodha wa Los Blancos Sergio Ramos amekuwa mstari wa mbele kuwaambia viongozi wa Madrid kuangalia sehemu nyingine, ambako kuna wachezaji ambao Zinedine Zidane anawahitaji.

OKWI NA BOCCO WAIPA SIMBA USHINDI MNONO DHIDI YA MWADUI

Simba imezidi kuchanja mbuga katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu baada ya kuifunga Mtibwa 3-0, Shukrani kwa John Bocco na Emmanuel Okwi
Simba imeburudisha mashabiki wake kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga katika mchezo wa Ligi Kuu Bara Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Nyota wa mchezo wa Jumapili kwa mara nyingine amekuwa mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi aliyefunga mabao mawili na kufikisha mabao sita katika mechi mbili tu za Ligi Kuu alizocheza msimu huu, kufuatia mabao manne katika ushindi wa 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye mchezo wa kwanza.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na waamuzi Emmanuel Mwandembwa, aliyesaidiwa na Joseph Masija na Michael Mkongwa, hadi mapumziko Simba walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Bao hilo lilifungwa dakika ya saba na Okwi aliyekosa mchezo uliopita wa Simba ikitoa sare ya 0-0 na Azam Jumamosi iliyopita Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam kutokana na kuchelewa kurejea baada ya kwenda kuichezea timu yake ya taifa, Uganda dhidi ya Misri mechi ya kufuzu Kombe la Dunia mwakani Urusi.
Okwi alifunga bao hilo kwa shuti la umbali wa mita 25 baada ya kumchungulia kipa wa Mwadui, Arnold Massawe aliyekuwa amesogea mbele kidogo kufuatia pasi ya winga Shiza Kichuya aliyekuwa anacheza kama kiungo zaidi.
Mwadui pamoja na kumiliki vizuri mpira walipopata nafasi, lakini hawakuwa na mipango kabisa ya kuipenya ngome imara ya Simba chini ya mabeki wa timu za taifa za Uganda na Tanzania, Juuko Murshid na Salim Mbonde.
Kipindi cha pili nyota ya Simba iliendelea kung’ara na dakika ya 67, Okwi tena akawainua vitini mashabiki wa Wekundu wa Msimbazi kwa kufunga la pili kwa shuti la umbali wa mita zisizopungua 20 baada ya pasi ya beki Mohammed Hussein ‘Tshabalala’.
Mashabiki wa Simba walizomea mabadiliko yaliyofanywa na kocha Mkameruni, Joseph Marius Omog mara mbili kwanza akimtoa Mghana Nicholaus Gyan na kumuingiza Mwinyi Kazimoto dakika ya 61 na baadaye akimtoa Kichuya na kumuingiza Mrundi, Laudit Mavugo dakika ya 65 wakionekana kabisa kutaka mshambuliaji John Bocco ndiye atolewe.
Bocco akawaonyesha mashabiki wa Simba kwamba Omog alikuwa sahihi katika mabadiliko yake kwa kufunga bao la tatu dakika ya 72 kwa shuti la umbali wa mita 20 na zaidi pia.
Mabao yote ya Simba yalikuwa mazuri na yenye kudhihirisha uwezo binafasi wa wachezaji kufunga na kwa ujumla, Wekundu wa Msimbazi walikuwa katika mechi nyepesi mno jioni ya Jumapili.
Sasa Simba wanakwenda kujiandaa kwa mechi inayofuata dhidi ya Mbao FC

LUKAKU: "KUSHANGILIA GOLI DHIDI YA EVERTON ILIKUWA MZAHA TU"

Romelu Lukaku ndiye mfungaji wa muda wote Everton, na alishangilia alipoifunga timu yake hiyo ya zamani lakini amesema alikuwa akifanya mzaha tu
Mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku amesisitiza kuwa kushangilia kwake baada ya kufunga dhidi ya Everton, klabu yake ya zamani ulikuwa ni mzaha tu.
Mshambuliaji huyo, 24, alijiunga na Man united akitokea Everton majira ya joto kwa dili linalokadiriwa kupanda hadi paundi milioni 90, alishika masikio yake na kuwanyooshe kidole mashabiki wa timu ya ugenini katika uwanja wa Old Trafford baada ya kufunga goli la tatu kwa klabu yake United wakishinda 4-0.
Vitendo vya Lukaku viliwakera mashabiki wa Everton, lakini Mbelgiji huyo amedai kuwa alikuwa akiwajibu mashabiki hao ambao walimzomea muda mfupi kabla.
"Ni goli jingine, kweli, lakini nafurahi tumeshinda na kuendelea kujiweka pazuri zaidi kuwania ubingwa," aliiambia Sky Sports News.
"Ulikuwa ni mzaha tu kidogo, baada ya kukosa mpira wa adhabu niliopiga walinizomea. Hili ni soka tu.
"Miaka bada ya miaka nafahamu kuwa nahitaji kuwa mvumilivu, kuendelea kujipanga na kuamini kuwa mpira utakuja mbele yangu, na kuendelea kujituma. Na kwa bahati njema mpira ulikuja mbele yangu.
Lukaku ambaye amfunga mabao saba, magoli yake mengi tangu atue United, ndiye mfungaji wa muda wote wa Everton katika Ligi Kuu Uingereza.

LUKAKU: "TUNGEWEZA KUFUNGA MAGOLI MENGI ZAIDI"

United walianza vizuri lakini walipoteza nafasi kadhaa za wazi licha ya goli la kwanza safi kutoka kwa Valencia, Everton walisababisha matatizo pia
Mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku amedai kuwa timu yao "haikuwa vizuri sana kwenye umaliziaji" licha ya kuifunga Everton kwa mabao 4-0 kwenye uwanja wa Old Trafford.
Mbelgiji huyo aliingia kwenye ubao wa wafungaji akifunga bao la tatu dhidi ya timu yake ya zamani United wakilingana pointi na mahasimu wao Manchester City ila tu kwa tofauti ya magoli kileleni mwa msimamo.
"Tungeweza kufunga zaidi nadhani kipindi cha kwanza. Lakini hatukuwa vizuri kwenye umaliziaji," Lukaku alikiambia Sky Sports News baada ya mechi. "Dakika 25 za mwanzo nadhani tulianza vizuri sana lakini baada ya hapo Everton walitusababishia matatizo zaidi kwenye eneo la kiungo.

ARSENE WENGER: 'DAVID LUIZ ALISTAHILI KADI NYEKUNDU'

Arsenal walicheza kiwango safi katika mechi yao ya ugenini wakipata sare ya 0-0 dhidi ya Chelsea David Luiz akipewa kadi nyekundu dakika za mwisho
Kikosi cha Arsene Wenger kimepoteza mechi zao zote za nyuma walizocheza ugenini msimu huu dhidi ya Stoke na Liverpool, lakini wangeweza kushinda pointi zote tatu Darajani, kwani Aaron Ramsey aligonga mwamba kipindi cha kwanza na goli la Shkodran Mustafi lilikataliwa kipindi cha pili.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amedai kuwa David Luiz wa Chelsea alistahili kadi nyekundu aliyopokea katika mechi hiyo ya Ligi Kuu Uingereza Stamford Bridge.
Luiz alioneshwa kadi nyekundu katika dakika za majeruhi kwenye mechi hiyo kubwa ya London na Michael Oliver baada ya kuruka vibaya dhdi ya beki wa Arsenal Sead Kolasinac.
Ni mara ya tatu mfululizo Chelsea wamepunguzwa kucheza watu kumi dhidi ya Gunners, ambao walipata sare ya 0-0 katika uwanja wa Stamford Bridge, lakini Wenger anaamini kuwa mwamuzi alifanya maamuzi sahihi.
"Alitumia nguvu nyingi, naam. Nadhani Kolasinac hakuwa amesimama kikamilifu kwa miguu yake. Hata Luiz mwenyewe atakubali kwamba kulikuwa na umbali mkubwa na alikwenda kwa nguvu," aliwaambia waandishi.
Luiz atafungiwa mechi tatu, hii ikimaanisha ataikosa safari ya Manchester City, pamoja na mechi dhidi ya Stoke City na Crystal Palace.
Chelsea wameshindwa kufunga katika mechi yenye ushindani katika uwanja wa nyumbani chini ya Conte kwa mara ya kwanza (mechi 27).

BALE NA MAYORAL WALIWEKA KIMIANI KUIREJESHA KWENYE NJIA ZA USHINDI RONALDO ANAPOJIANDAA KURUDI

Winga huyo raia wa Wales akiwa katika kiwango cha juu alifunga bao safi katika uwanja wa Anoeta pamoja na kinda wa Kihispania akifanya kazi nzuri pia
Gareth Bale anapenda kucheza katika uwanja wa Anoeta. Mchezaji huyo, 28, amekuwa akizomewa na mashabiki wa Real Madrid katika uwanja wa Santiago Bernabeu siku za hivi karibuni, lakini aliwapatia zawadi mahususi ugenini dhidi ya Real Sociedad. Alifanya kazi nzuri Jumapili na akishirikiana na Borja Mayoral waliirejesha Los Blancos kwenye njia za ushindi La Liga.
Kufuatia sare dhidi ya Valencia na Levante nyumbani Madrid walipoteza pointi nne kwenye mechi za La Liga hivyo kuiruhusu Barcelona kuongeza pengo la pointi dhidi yao.
Wakiwa wamepungukiwa nguvu ya mashambulizi mechi mbili zilizopita Zidane alikiri kuwa angependa kusajili mshambuliaji mwingine baada ya Alvaro Morata kuuzwa Chelsea, lakini Mfaransa huyo alimpa Mayoral nafasi ya kuanza Jumamosi pembeni ya Marco Asensio na Bale katika safu ya mashambulizi.
"Labda tunaweza kufanya vizuri tukipata namba 9 mwingine, lakini huu si mwisho," alisema wiki iliyopita. "Morata alitaka kucheza zaidi, alitaka kuondoka. Hatukuweza kuleta mchezaji mwingine, lakini namwamini [Borja] Mayoral, lakini pia tunaye Gareth. Ni kweli anacheza zaidi kama winga lakini anaweza."
Na ndivyo ilivyokuwa. Mayoral alifungua ukurasa wa mabao, akimalizia viuzri kabisa, na pia aliwalazimisha Sociedad kujiunga kipindi cha kwanza baada ya wapinzani wao kusawazisha kupitia Kevin Rodriguez, ambaye pia shuti lake lilizuiliwa na Keylor Navas.
Isco pia alicheza katika kiwango bora akipiga pasi ndefu na nzuri akimpa pande Bale, ambaye alikimbia yadi 73 na kumpita Kevin kwa kasi ya ajabu na kumfunga mlinda mlango Geronimo Rulli.
Madrid wamepata ushindi wa 11 mfululizo ugenini kwa mara ya kwanza katika historia yao na Los Blancos sasa wamefunga katika mechi zao 73 za mwisho kufikia rekodi iliyowekwa na Santos ya Pele.

NEYMAR AKIMBIA KUPIGA PENALTI PSG - LAKINI CAVANI AMZUIA

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay alikuwa king'ang'anizi akitaka kupiga penalti dhidi ya Lyon lakini aliishuhudia ikiokolewa
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazili alitembea kwenda kupiga penalti waliyopata PSG dakika ya 78 mechi ya Jumapili Ligue 1 dhidi ya Lyon, timu ya Unai Emery ikiwa inaongoza kwa bao 1-0.
Lakini Edinson Cavani alikuwa ameshawahi, na mshambuliaji huyo wa Uruguay alimwambia Neymar aondoke kabla ya kurudi nyuma kupiga penalti ambayo hata hivyo iliokolewa na kipa wa Lyon Anthony Lopes.
Kwa mashindano yote hayo, hatimaye PSG waliondoka na pointi tatu ambapo amgoli kutoka kwa wachezaji hao wawili yaliwawezesha kushinda 2-0.

MANCHESTER CITY WAISAMBARATISHA WATFORD

Manchester City wamekwea hadi kileleni mwa msimamo wa ligi ya Uingereza baada ya kujipatia ushindi wa 6-0 dhidi ya Watford Jumamosi Vicarage Road
Sergio Aguero aliendeleza rekodi yake dhidi ya Watford kwa kufunga mabao matatu, pamoja na magoli kutoka kwa Gabriel Jesus, Nicolas Otamendi na Raheem Sterling aliyefunga kwa penalti kukamilisha karamu ya mabao.
Watford walijipanga vizuri kwenye eneo lao katika kipindi cha kwanza, na walikaribia kupata bao la kuongoza dakika ya 26 kupitia mpira wa kichwa uliopigwa na Richarlison baada ya kupokea mpira wa adhabu ndogo kutoka kwa Jose Holebas.
Hata hivyo Watford walibana na waliachia baada ya dakika moja, mpira adhabu kutoka kwa Kevin De Bruyen ulimfikia Aguero moja kwa moja na aliunganisha kwa kichwa hadi wavuni.

LIVERPOOL WAVURUGWA NA BURNLEY KWA SARE ANFIELD

Mohamed Salah alisawazisha goli la Scott Arfield la dakika ya 27, lakini Reds hawakuweza kushinda licha ya kutawala mchezo kikamilifu
Wiki ya Liverpool imekuwa mbaya zaidi ya awali kufuatia sare ya 1-1 dhidi ya Burnley katika uwanja wao wa nyumbani Anfield.
Waliumizwa na sare ya Sevilla Ligi ya Mabingwa Jumatano, na pia walichapwa 5-0 na Manchester City wikiendi iliyopita.
Philippe Coutinho alirejea kwenye kikosi cha Liverpool baada ya kupata uhamisho kwenda Barcelona alikokuwa akipatamani na alipiga mpira mwingi katika hatua za mwanzo Liverpool ilipoanzisha mashambulizi dhidi ya beki ya wapinzani.

LIONEL MESSI AJIFUNGA BARCELONA HADI 2021

Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu amebainisha kuwa baba wa Lionel Messi amesaini mkataba mpya kwa niaba ya Mwargentina huyo hadi 2021
Klabu hiyo ya La Liga ilitangaza Julai kuwa Messi amekubali mkataba mpya wa miaka minne na ilikuwa mkataba usaini baada ya wiki chache Messi atakaporudi kutoka kwenye maandalizi ya msimu.
Tangu hapo hapakuwa na tamko rasmi na tetesi ziliendelea kusambaa kuhusu mustakabali wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30.
Bartomeu, sasa, amezungumza kupitia televisheni ya Catalan kuthibitisha kuwa mshindi huyo wa mara tano wa Ballon d'Or Messi amejifunga Nou Camp kwa mkataba mpya.

NGOMA AINUSURU TENA YANGA NA KIPIGO

Yanga imezidi kujikongoja kutetea ubingwa wake baada ya leo kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Majimaji ya Songea
Mshambuliaji wakimataifa wa Zimbabwe Donald Ngoma, leo ameinusuru timu yake ya Yanga na kipigo kutoka kwa Majimaji baada ya kuifungia bao la kusawazisha dakika ya 79 akiunganisha krosi iliyopigwa na Mzambia Obrey Chirwa katika pambano la Ligi ya Tanzania Bara lililopigwa uwanja wa Majimaji Songea.
Hiyo ni mara ya pili kwa Ngoma kuinusuru Yanga kwa kipigo msimu huu, mara ya kwanza ilikuwa kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Lipuli FC, uliochezwa uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, lakini yeye aliisawazishia timu hiyo dakika tatu kabla timu hizo hazijaenda mapumziko.
Majimaji ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza lililofungwa na Peter Mapunda dakika ya 54, kufuatia pasi nzuri ya kiungo Abdulihalim Humud.
Sare hiyo inaifanya Yanga kufikisha pointi 5 wakati Majimaji wanafikisha pointi mbili hivyo kuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha wanapambana na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufanya vizuri kwenye ligi ya msimu huu.
Katika mchezo huo wenyeji Majimaji waliuanza mchezo kwa kasi na kufanya mashambulizi mengi kwenye lango la Yanga lakini mabeki wa Yanga walikuwa imara na kuondosha hatari zote langoni mwao.
Yanga ilizinduka na kuanza kupanga mashambulizi yake vizuri lakini ubovu wa uwanja ilikuwa kikwazo kwa timu zote hasa Yanga ambao wamezoea kucheza kwenye uwanja wa Uhuru au ule wa Taifa Dar es Salaam, ambavyo vinanyasi halisi na kingine bandia.
Hadi mapumziko timu hizo zilikuwa sare ya bila kufungana huku umiliki wa mpira ukiwa 50-50, lakini Yanga walitengeneza nafasi nyingi za kufunga kuliko wenyeji wao Majimaji ambao walikuwa akicheza kwa kujihami huku wakitumia mashambulizi ya kustukiza.
Kipindi cha pili kocha wa Majimaji Habibu Kondo, aliwaingia wachezaji wakongwe Jeryson Tegete na Abdulihalim Humud, ambao walionekana kuongeza nguvu na kasi ya mashambulizi kwenye lango la Yanga.
Katika dakika ya 48 ya mchezo mshambuliaji Ibrahim Ajibu wa Yanga alipoteza nafasi ya wazi kuifungia timu yake bao la kusawazisha baada ya kushindwa kumalizia krosi iliyochongwa na Geofrey Mwashiuya na kipa Endrew Ntala alifanya kazi nzuri ya kupangua mpira huo.
Baada ya kuingia kwa bao hilo Yanga walizinduka na kuzidi kupambana kwa kumiliki mpira lakini Majimaji walikuwa makini kwenye kujilinda na kuondosha hatari langoni mwao.
Pamoja na kufanya mashambulizi mengi bila kupata bao kocha George Lwandamina aliamua kumtoa Juma Abduli na kumuingiza Hassani Kessy ambaye alisaidia kupandisha mashambulizi mbele na kupiga krosi nyingi langoni mwao.
Jitihada za Yanga ziliweza kuzaa matunda dakika ya 79, ambapo Ngoma aliunganisha kwa kichwa mpira uliopigwa na Chirwa na kusawazisha bao hilo ambalo lilikuwa likisubiriwa kwa hamu na mashabiki wao ambao muda wote wa mchezo alikuwa kimya.
Kuingia kwa bao hilo kuliwaongezea kasi ya mashambulizi Yanga na kuliandama lango la Majimaji, lakini wapinzani wao alicheza kwa umakini huku wakitumia mbinu ya kujiangusha kupoteza muda ili kupata ushindi.
Katika dakika ya 85, mchezaji wa Yanga Emmanuel Martin alilazimika kutolewa nje, baada ya kupoteza fahamu kufuatia kugongana na mchezaji wa Majimaji, lakini baadaye madaktari wa timu hiyo walimpa huduma ya kwanza na kurudi kwenye hali yake ya kawaida.
Yanga imemaliza mechi za kanda ya Kusini kwa kupata pointi nne, baada ya ushindi wa bao 1-0, walioupata Jumamosi iliyopita dhidi ya Njombe Mji ya Njombe na Jumamosi ijayo watakuwa nyumbani uwanja wa Uhuru kucheza na Ndanda FC ya Mtwara.

TIMU YA TAIFA YA TANZANIA YA WASICHANA U-20 IMEJIWEKA KATIKA MAZINGIRA MAGUMU KUFUZU KOMBE LA DUNIA



Kocha Sebastian Nkoma na vijana wake wanaitaji jitihada kubwa ili kuweza kusonga mbele kwenye mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo hapa nchini
Timu ya Taifa ya Tanzania ya wanasichana wenye umri wa chini ya miaka 20 ‘The Tanzanite’ imeanza vibaya harakati zake za kufuzu kombe la Dunia mwakani nchini Ufaransa.
Timu hiyo ya wasichana "The Tanzanite imekukubali kipigo cha magoli matatu kwa bila dhidi ya Nigeria, mechi iliyopigwa kwenye uwanja wa Samuel Ogbemudia uliko Jiji la Benin.
Mchezo huo wa awali ulikuwa ni kwa ajilii ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia kwa wasichana wenye umri wa chini ya miaka 20, michuano ambayo itafanyika mwakani nchini Ufaransa.
Kwa matokeo hayo, Tanzania imejiweka katika mazingira magumu kwenye mechi ya marudiano wiki mbili zijazo hapa nchini, kwani wanaitaji kushinda zaidi ya goli nne ili kupata tiketi ya kufuzu michuano hiyo.
Kikosi cha Tanzania maarufu kama Tanzanite kinaundwa na makipa Agatha Joel, Zainab Abdallah na Gelwa Mgomba Walinzi ni Eva Jackson, Aquila Gasper, Asphat Kasindo, Ester Mayala, Silivia Mwacha,  Stella Wilbert, Wema Richard,  Hadija Ali, Rukia Anafi na Christine Daudi. Viungo ni Herieth Shija, Julieth Singano na Shamimu Hamis huku Washambuliaji ni Veronica Mapunda, Opa Clement, Zainabu Mohamed na Philomena Daniel.https://www.qsport2017.blogsport.com

GUARDIOLA AMPA ONYO MBAPPE

Nyota huyo kinda amefurahia mwanzo mzuri katika soka, lakini Bosi wa Manchester aliyewahi kuinoa Barcelona amesema hilo halina maana amefanikiwa
Pep Guardiola amekataa kubashiri kama Kylian Mbappe atafikia anga za Lionel Messi, lakini ameonya "hakuna mtu anayeweza kukaa meza moja" na nyota huyo wa Barcelona.
Manchester City ya Guardiola ni miongoni mwa klabu zilizokuwa zikiifuatilia saini ya Mbappe baada ya kung'ara Monaco msimu uliopita - baada ya kinda huyo kufunga katika kila mechi kwenye hatua ya 16-bora ambapo klabu hiyo ya Ligue 1 ilishinda kwa mbao ya ugenini kufuatia sare ya 6-6.
Mbappe alifunga magoli 26 katika mechi 44 Monaco ikiipiku Paris Saint-Germain kutwaa taji la Ligue 1 na kufika nusu fainali Ligi ya Mabingwa.

MANCHESTER UNITED KUELEKEA MCHEZO DHIDI YA EVERTON

Jose Mourhino amethibitisha kiungo wa Manchester United, Paul Pogba atahukosa mchezo wa Jumapili dhidi ya Everton kutokana na kuuguza majeraha
kiungo Mfaransa alichaguliwa kuwa kapteni kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya FC Basel, lakini alitolewa kwenye kipindi cha kwanza kutokana na tatizo la misuli. Nafasi yake ilichukuliwa na Maroune Fellaini na Mbelgiji huyo alionesha thamani yake, alifunga goli  na kusaidia lingine la Marcus Rashford.
Akizungumza na MUTV wakati wa mahojiano katika Complex Aon Training,Jose alianza kwa kutoa taarifa juu ya afya ya Pogba. "Ni mejeruhi na hawezi kucheza siku ya Jumapili," meneja alituambia.
Mourihno amesema hajui kwa muda gani Pogba atakuwa nje na baadaye aliongeza: "Tunajua kwamba, kwa mechi chache, sijui ngapi, lakini natarajia tutacheza bila Pogba kwa mechi chache "Hata hivyo, Jose alikuwa na nia ya kusisitiza kutokuwepo kwake ni fursa nzuri kwa kikosi kimoja kupambana.

CONTE: N'GOLO KANTE NI MCHEZAJI MWENYE UWEZO MKUBWA

ndondo2017.blogspot.com

N'Golo Kante amekuwa mchezaji muhimu kwenye kikosi cha Chelsea, na Conte amekiri kuwa mchezaji huyo anaimarika kila kukicha
Meneja wa Chelsea Antonio Conte amedai kuwa N'Golo Kante amethibitisha kuwa yeye ni mchezaji bora wa anga nyingine wiki za kwanza katika Ligi Kuu Uingereza.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alikuwa mchezaji bora wa mwaka wa tuzo za PFA 2016-17 baada ya kuisaidia Chelsea kupata mafanikio, miezi 12 tu baada ya kufanya hivyo akiwa Leicester City.
Kante aling'ara kwa mara nyingine mabingwa hao watetezi wakishinda 2-1 dhidi ya Leicester katika uwanja wa King Power, Conte hakuweza kuficha furaha yake kuhusu nyota huyo.
"N'Golo ni mchezaji muhimu sana kwetu - mchezaji mkubwa," aliwaambia waandishi. "Kilikuwa ni kiwango cha kuvutia. Alicheza soka safi sana. Alifunga lakini bado alifanya kazi kubwa sana. Kila siku anaimarika. Nadhani anakuwa bora zaidi akiwa na mpira.
"Hapo mwanzo, watu wengi waliniambia, 'Ni mchezaji mzuri bila ya mpira, ana stamina na mchapakazi', lakini sasa ni mzuri akiwa na mpira pia."
Chelsea ambao wameshinda mechi tatu mfululizo na kupanda hadi nafasi ya tatu msimamo wa Ligi ya Uingereza, watashuka dimbani tena wiki hii kuikabili Qarabag kwenye Ligi ya Mabingwa.

MANCHESTER UNITED YAANZA NA USHINDI LIGI YA MABINGWA ULAYA

ndondo2017.blogspot.com
Manchester United imefungua kampeni zake kwenye Ligi ya mabingwa ulaya kwa ushindi wa goli 3 kwa bila.
United, ambaye amerejea kwenye ushindani wa klabu bingwa ulaya baada ya kukosekana kwa mwaka mmoja baada ya kushinda kombe la Europa msimu uliopita, walimpoteza kwa majeruhi kipindi cha kwanza lakini mabadala wake Fellaini alikuja kuleta madhara makubwa, alifunga goli la kwanza dakika ya 35
Romelu Lukaku aliongeza lingine dakika ya 53 kabla ya mtokea benchi Rashford kuja kuhakikisha alama tatu kwa vijana wa Jose Mourihno.
Pogba alizawadia kitambaa cha ukapteni na Mourihno lakini alicheza kwa dakika 19 tu na Mfaransa huyo kuumia kama kifundo cha mguu.

CHELSEA YAIDHALILISHA QARABAG KWA KIPIGO CHA MABAO 6-0 UEFA

ndondo2017.blogspot.com
Chelsea wameanza kampeni za Ligi ya Mabingwa kwa ushindi mnono wa 6-0 dhidi ya Qarabag FK ya Azerbaijani
Blues walitawala mchezo mwanzo mwisho katika uwanja wa Stamford Bridge, Pedro, Davide Zappacosta, Cesar Azpilicueta, Tiemoue Bakayoko wote wakiingia kwenye ukurasa wa mabao kabla ya Maksim Medvedev kujifunga.
Iliwachukua dakika nne tu Chelsea kutengeneza nafasi yao ya kwanza katika mechi hiyo Marcos Alonso akikataliwa shuti la umbali wa yadi 14, lakini muda mfupi baadaye Pedro aliwainua vitini mashabiki wa Chelsea kwa bao bora kabisa.
Qarabag walitanda kote katika eneo lao la nyuma kuwathibiti wapinzani wao, lakini vijana hao wa Gurban Gurbanov pamoja na jitihada zao, walikuwa walaini mbele za Chelsea.

PAUL POGBA APATA MAJERAHA MAN UNITED IKISHINDA DHIDI YA BASEL


ndondo2017.blogspot.com
Mechi ya kwanza ya Paul Pogba kama nahodha wa Manchester United ilidumu kwa muda wa dakika 18 tu baada ya kupata majeraha dhidi ya Basel
Meneja wa Manchester United amesema hajui ni kiasi gani mchezaji huyo amepata majaraha baada ya mchezo, lakini Mfaransa huyo alitoka Old Trafford akiwa anaugulia maumivu.
"Kwa kweli sijui, lakini kwa uzoefu wangu, kwa kuangalia tu nahisi ni majeraha ya misuli," Mourinho alisema. "Jeraha kubwa, dogo, sijui."
Michael Carrick na Antonio Valencia wakiwa benchi, Pogba alirithi kitambaa cha unahodha katika uwanja wa Old Trafford, lakini haikuwa siku yake nzuri kwa sababu ya majeraha hayo.

GOLI LA MAROUANE FELLAINI DHIDI YA BASEL LATHIBITISHA UMUHIMU WAKE

ndondo2017.blogspot.com
Marouane Fellaini ameonyesha ni kwa nini bado ni mchezaji muhimu kwenye kikosi cha Manchester United baada ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Basel
"Namhitaji." Hayo yalikuwa maneno ya Jose Mourinho kuhusu Marouane Fellaini kabla ya mechi ya Manchester United Ligi ya Mabingwa dhidi ya Basel Jumanne.
Haikumchukua muda mrefu kiungo huyo kuonesha ni kwa nini anahitajika, akiingia kutokea benchi baada ya Paul Pogba kupata majeraha dakika ya 18 ya mchezo aliipatia bao la kwanza United iliyoshinda 3-0 Old Trafford.
Fellaini alionesha vitu vingi zaidi ya goli alilofunga. Alimsaidia Nemanja Matic alipopoteza mpira katika mazingira ya hatari, lakini pia alipiga krosi maridadi kwa Marcus Rashford aliyefunga ukurasa wa mabao dhidi ya Basel.

LIONEL MESSI AIONGOZA BARCELONA KUISULUBISHA 3-0 JUVENTUS

ndondo2017.blogspot.com
Michuano ya Ligi ya Mabingwa imeanza kwa ushindi kwa Manchester United, Barcelona, PSG na Chelsea, Messi akiendelea kutoa burudani ya soka
Lionel Messi alitikisa nyavu mara mbili Barcelona ikitoka kifua mbele kwa ushindi wa 3-0 dhidi ya Juventus mechi ya kwanza Ligi ya Mabingwa msimu wa 2017-18, kadhalika Paris Saint-Germain, Manchester United na Chelsea zilipata ushindi mnono Jumanne.
Baada ya msimu wa majira ya joto uliojaa adha tele, Barca walikabiliana na mshindi wa pili wa michuano hiyo msimu uliopita, huenda hawakucheza katika kiwango walichotaka kama timu, lakini Lionel Messi alidhihirisha umahiri wake akiiwezesha Blaugrana kushinda pointi tatu muhimu.
Mchezaji mpya Ousmane Dembele alipewa nafasi kikosi cha kwanza Camp Nou, lakini ni Messi aliyeweka kimiani bao la kufungua ukurasa baada ya kugongeana vema kabisa na Luis Suarez.

ARSENE WENGER: "KYLIAN MBAPPE NDIYE PELE MPYA"

ndondo2017.blogspot.com
Pele ni mchezaji mwenye wasifu mkubwa katika historia ya mchezo wa soka, na Arsene Wenger anaamini Mbappe atafanya maajabu kama Mbrazili huyo
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amemwagia sifa mshambuliaji wa Paris Saint-Germain Kylian Mbappe, akidai kuwa Mfaransa huyo anaweza kuwa "Pele mpya".
Arsenal walikuwa miongoni mwa klabu nyingi zilizokuwa zikitaka saini ya Mbappe majira ya joto baada ya mchezaji huyo kuwika akiwa na Monaco iliyotwaa taji la Ligue 1.
PSG wameshinda mbio za saini ya mchezaji huyo kwa dau nono la fedha, na baada ya nyota huyo kinda kufunga katika mechi yake ya kwanza klabuni hapo, Wenger hakuona sababu ya kutomsifia.
"Nadhani ni mchezaji mwenye akili ya kipekee, anatabia ya kipekee na imani ya kipekee," Wenger alikiambia BeIN Sports.
"Nawaambia rafiki zangu, 'Mbappe ndiye Pele mpya'. Anaweza kuwa mchezaji bora duniani, kwa sababu ana haiba, tabia njema na imani njema.
"Huwezi kudhani unazungumza na mtu wa miaka 18 unapoongea naye. Daima huonyesha uwezo mkubwa anapokuwa na mpira na jambo lolote linaweza kutokea."
Mbappe amefunga mabao 26 katika mechi 44 akiwa Monaco msimu uliopita, na hivi sasa amefungua akunti yake ya mabao Ufaransa pia.

NYOTA BORA WA WIKI

Yakubu Mohammed alikuwa kikwazo kwa upande wa Simba kushindwa kuondoka na alama tatu
Mlinzi wa kati wa klabu ya Azam, Yakubu Mohammed amefanikiwa kuwa mchezaji bora wa wiki baada ya kuwa katika kiwango bora kwenye mechi dhidi ya Simba.
Azam na Simba waligawana pointi kwenye mchezo uliomalizika  kwa sare ya bila kufungana siku ya Jumamosi kwenye uwanja wa Chamanzi.
Yakubu Mohammed ameibuka nyota wa wiki baada ya kuwazidi wachezaji kadhaa waliokuwa na wikendi nzuri kama James Kotei, Ibrahim Ajibu, Marcel Kaheza na wengineyo.
Yakubu alikuwa kikwazo kwa upande wa Simba  kushindwa kuibuka na alama tatu licha ya kusheheni nyota wenye uwezo mkubwa, Yakubu alifanikiwa kuziba mianya yote hatari, alikuwa bora kwa mipira ya juu na ya chini mbele ya mastraika wa Simba John Bocco na washambuliaji wengine wa Mnyama.
Katika hatua nyingine pia Mghana huyo alikuwa bora kwenye matumizi ya nguvu hasa kwenye mipira ile ya kugombea dhidi ya wapinzani wake siku hiyo.

Alichofanyiwa Rudiger na shabiki wa Chelsea

Kufatia mchezo wa jana kati ya Man city na Chelsea, Chelsea kuambilia kipigo cha goli 6, baada ya mchezo kumalizika mlinzi huyo wa kat...

Most viewed